Aliyesimama
ni Mwenyekiti wa Taifa wa umoja wa wasambazaji wa kazi za Sanaa nchini,
yaani ‘Tanzania Audio Visual Works Distributors,’ Baraka Nyanda
akiongea na waandishi wa habari jijini Arusha juu ya kushuka kwa ubunifu
miongoni mwa wasanii nchini ambako kumepelekea uwepo wa sinema na
miziki hafifu isiyoweza kusahimili ushindani wa soko la kazi za burudani
duniani anayefatia ni katibu wa shirika hilo Frank Martin ,watatu ni
James Mollel katibu tawi laArusha pamoja na Gabriel Simbeye mjumbe.
katibu wa
shirika la Tanzania Audio Visual Works Distributors Frank Martin
amebainisha kuwa tasnia ya filamu na muziki nchini ilikuwa na mafanikio
kuanzia mwaka 2005 ambapo kazi Zaidi ya 300 zilikuwa zinafyatuliwa kila
mwaka kwa mujibu wa ripoti ya Media for Development International ya
2011.
Mwandishi wa habari kutoka Daily News Marc Nkwame akiuliza swali.(VICTOR)
Simon
Mwapangala maarufu kama ‘Rado,’akizungumzia hali halisi ya kushuka kwa
soko la sanaa hapa Nnchini ambapo alisema kuwa hata kampuni za
usambazaji filamu zinachangia kuua tasnia hiyo kwa kuwapa waandaaji
malipo finyu.
Muziki na
Filamu zinazorekodiwa nchini zinadaiwa kupoteza umaarufu nchini kiasi
cha kusababisha soko lake kuangukia pua, huku waandaaji na wasambazaji
wake wengi wakiamua kujitoa na kutafuta shughuli zingine za kufanya.
Mwenyekiti
wa Taifa wa umoja wa wasambazaji wa kazi za Sanaa nchini, yaani
‘Tanzania Audio Visual Works Distributors,’ Baraka Nyanda, pamoja na
katibu wa shirika hilo Frank Martin wamelaumu kushuka kwa ubunifu
miongoni mwa wasanii nchini ambako kumepelekea uwepo wa sinema na miziki
hafifu isiyoweza kusahimili ushindani wa soko la kazi za burudani
duniani.
“Tathmini
kutoka wasambazaji waliochini ya ‘Tanzania Audio Visual Works
Distributors,’ ambao wanafikia 200 kwa sasa, imeonesha kupungua kwa kazi
za Sanaa yaani muziki na filamu kwa asilimia Zaidi ya 50 na hii
imesababishwa na kukosekana kwa masoko ya kazi hizo nchini,” alisema
Katibu wa chama hicho, Frank Martini.
0 comments:
Post a Comment